http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Ruge athibitisha Makonda kuivamia Clouds media akiwa na silaha

Mkurugenzi wa Vipindi na Uendeshaji wa Kituo cha Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amehojiwa leo katika kipindi cha 360 cha televisheni ...


Mkurugenzi wa Vipindi na Uendeshaji wa Kituo cha Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amehojiwa leo katika kipindi cha 360 cha televisheni ya Clouds na kuthibitisha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda alivamia kituo hicho..


Akizungumza na watangazaji wa kipindi hicho, Ruge aliongea kwa hisia na kuthibitisha kuwa tukio hilo lilitokea siku ya ijumaa ya tarehe 17 majira ya usiku kituoni hapo.


Alieleza kuwa, siku ya Alhamisi RC makonda alifika katika kituo hicho na kuongea na watangazaji wa SHILAWADU, Sudy Brown na Qwisser ambapo alisema kuwa wanapiga tu stori.


“Mtangazaji mmoja alinifuata akaniambia wamefanya mahojiano na mwanamke anayedaiwa kuwa amezaa na Askofu Gwajima lakini Gwajima mwenyewe hawajampata. Niliwaambia watangazaji kama hawajampata Gwajima, basi kipindi hicho kisirushwe kwa kuwa hakina ‘balance’ na wamwambie Makonda.”


“Gwajima alinipigia simu akisema amesikia kuwa kuna kipindi chake, nikamwambia kuwa hakitarushwa kwa sababu hatujasikia pande zote. Na nikampigia simu mkuu wa vipindi kumwambia ahakikishe kuwa kipindi hicho hakirushwi kwa vile hakijabalance.”


“Ijumaa saa 5 usiku nikapigiwa simu na Afisa Rasilimali Watu wa Clouds kuwa Makonda amekuja ofisini akiwa na Askari na wana bunduki. Mlinzi hakusita kumruhusu aingie kwa vile amemzoea Makonda, ila alishtushwa na Askari wale waliokuwa na Bunduki.”


“Nilimwambia mlizi aende juu studio aone kuna nini na alipokwenda alimkuta Makonda anachukua kipindi kwenye ‘flash’ kisha akaondoka nayo. Hakuna kijana yeyote aliyepigwa usiku ule lakini tatizo kubwa ni namna tukio zima lilivyotokea.”


“Makonda alikuja pale na Askari baada ya kuona kipindi chake hakirushwi, hivyo ni kama alikuja kuhoji sababu za kutorushwa kwa kipindi hicho.” Alisema Ruge Mutahaba wakati wa mahojiano leo asubuhi.


Akizungumza kuhusu video za kamera za ulinzi (CCTV) zilizosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, Ruge alikiri kuwa video hizo ni za Clouds lakini hajui ni nani alizitoa kwa sababu wafanyakazi wengi wanafahamu mitambo ya CCTV ilipo hivyo yeyote anaweza kutoa.


Vilevile Ruge ameeleza kuwa amesikitishwa sana na kitendo alichokifanya rafiki yake Paul Makonda kwani kilikuwa ni kitendo cha kuivunjia heshima Clouds Media Group pamoja na wadau wengine.

“Makonda tumesaidiana sana tangu akiwa mkuu wa Wilaya. Kwa nini leo anafika kuja ofisini kwangu na bunduki?” alisema.


“Makonda ni mkuu wa mkoa wa Dar es salaam lakini ni mdogo sana kwangu kiumri, lazima tuheshimiane. Sijayasema haya kwa sababu nataka mtu atumbuliwe, bali nataka heshima kwenye kile tunachokifanya.”


“Sasa tunakuwa tunampa Rais Magufuli mambo mengine ya kufanya ambayo hakutakiwa kuwa anayawaza.”


Pamoja na hayo aliongeza kuwa, wao kama Clouds Media Group hawana ugomvi na serikali na ameahidi kutoa nafasi kwa kiongozi yeyote mwenye ajenda ya maendeleo kuja Clouds na atapewa muda wa kuzungumza.

“Sisi tunatafuta viongozi wabunifu. Viongozi wanaokuja na mipango inayoweza kumwezesha mnyonge kuuona mwanga. Viongozi wanapaswa kufanya mijadala ya namna ya kuongeza maendeleo. Inapaswa tushirikiane kutengeneza timu moja na kushirikiana.”


Mkurugenzi Ruge Mutahaba, alimaliza kwa kusema kuwa amelizungumzia jambo hilo leo ili limalizike na watu waendelee kufanya mambo mengine ya kuisaidia nchi kimaendeleo.

Vilevile amewataka viongozi na wanasiasa kutokushindana kupata ‘kiki’ kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Ruge athibitisha Makonda kuivamia Clouds media akiwa na silaha
Ruge athibitisha Makonda kuivamia Clouds media akiwa na silaha
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-HQku-VUVTCSRF6PNsIsfqy5WoUdkGSMNVkAJNVnnGQ-dTVVx_ZyMjzm3v7Vsw_Q8fxXi6OpLJBm-jAzFHBXTtB5WHSjjxfRE4CsFcvqOwlLZnItZsrQ_-X7IvozvaAJQ7T2hxit5MQRI/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-HQku-VUVTCSRF6PNsIsfqy5WoUdkGSMNVkAJNVnnGQ-dTVVx_ZyMjzm3v7Vsw_Q8fxXi6OpLJBm-jAzFHBXTtB5WHSjjxfRE4CsFcvqOwlLZnItZsrQ_-X7IvozvaAJQ7T2hxit5MQRI/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/ruge-athibitisha-makonda-kuivamia.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/ruge-athibitisha-makonda-kuivamia.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy