http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mtu Mmoja Afariki Jijini Dar es Salaam......Jeshi la Polisi Latoa Tahadhari

Na Regina Mkonde Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam jumanne ya Machi 13, 2017 katika eneo la Mongo la Ndege, limeokota mwili ...


Na Regina Mkonde
Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam jumanne ya Machi 13, 2017 katika eneo la Mongo la Ndege, limeokota mwili wa mtoto wa kike aliyefahamika kwa jina la Imelda Ngonyani (13) aliyekufa maji wakati akijaribu kuvuka mto Msimbazi.


Akizungumza na waandishi wa habari Machi 14, 2017, Kamishna wa Kanda hiyo, Kamanda Simon Sirro amesema marehemu huyo kabla ya kufa maji alikuwa pamoja na wenzake watano walionusurika kifo wakielekea shule ya Msingi ya Mongo la Ndege.


“Mwanafunzi huyo alikufa maji wakati akijaribu kuvuka mto Msimbazi akiwa na wenzake ambao walinusurika kifo wakiwa njiani kuelekea shule ya Mongo la Ndege,” amesema.


Sirro ametoa wito kwa wananchi kuwa makini katika kipindi hiki cha mvua za masika zinazoendelea kunyesha, na kuwataka wananchi wanaoishi karibu na mto msimbazi kuondoka kwa hiari ili kujiepusha na athari za mafuriko.


Katika hatua nyingine, Kamanda Sirro amesema Jeshi la Polisi mnamo Machi 12, 2017 maeneo ya Zimbwini kata ya Vijibweni Manispaa ya Kigamboni lilifanikiwa kukamata watuhumiwa wawili wenye umri kati ya 25 hadi 30 wakiwa na bastola moja aina ya Bereta yenye risasi sita ndani ya magazini.


“Majambazi hao walijeruhiwa vibaya ndipo wakakimbizwa hospitali ya vijibweni, walipofikishwa hospitalini hapo walibainika kuwa wamefariki dunia wakiwa njiani. Uchunguzi wa awali umebaini kuwa silaha hiyo iliyokamatwa ni mali ya Pato Sixtus Nyagali mkazi wa Kijichi, upelelezi unaendelea kufanyika ili kumpata mmiliki huyo na kuhakikisha mtandao wote wa uhalifu unafikishwa katika mkono wa sheria,” amesema.


Sambamba na hilo, Sirro amesema Kikosi cha Polisi Usalama Barabarani cha kanda hiyo, kimekusanya 319,350,000 za faini kwa ajili ya makosa mbalimbali ya barabara kuanzia Machi 10 hadi 13, 2017.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mtu Mmoja Afariki Jijini Dar es Salaam......Jeshi la Polisi Latoa Tahadhari
Mtu Mmoja Afariki Jijini Dar es Salaam......Jeshi la Polisi Latoa Tahadhari
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6Oyi35hyphenhyphenQiCUsjw20RBIKQRxDcrxYJ9u59HhhmIfPzAKSHDIZJCQO8Uia7fuPIb-IiizzvGAK2zhg-umxhMg01wVmOhEbj39PzgZ6g5G0Oq1rnDWbqAGVXR0ey1hobhyphenhyphenclHhcahZNQ4FG/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEg6Oyi35hyphenhyphenQiCUsjw20RBIKQRxDcrxYJ9u59HhhmIfPzAKSHDIZJCQO8Uia7fuPIb-IiizzvGAK2zhg-umxhMg01wVmOhEbj39PzgZ6g5G0Oq1rnDWbqAGVXR0ey1hobhyphenhyphenclHhcahZNQ4FG/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/mtu-mmoja-afariki-jijini-dar-es.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/03/mtu-mmoja-afariki-jijini-dar-es.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy