http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

SIRRO:NINAUSONGO NA WALE WANAOFANYA FUJO ILI NIWASHUGHULIKIE KISWASWA

Na,Vero Ignatus ,Dar- es -salaam. Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Sirro amesema kuwa anausong...



Na,Vero Ignatus ,Dar- es -salaam.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna wa Polisi Simon Sirro amesema kuwa anausongo na watu ambao watakaofanya fujo katika uwanja wa taifa watakaokwenda kutazama mechi kati ya simba na yanga ili awashughulikie kisawasawa

Ametoa rai hiyo alipokuwa akizungumza kwenye kituo cha East Africa Radio na kusema kuwa atakayekwenda kutazama mechi jumamosi ya tarehe 25 februari 2017 aingie salama na atoka salama bila kugusa kiti atakayekiuka sheria itafuata mkondo wake.

"Nasema hivi mama kama mwanao ni mtukutu bora umwambie asije uwanjani kabisa,mama kama mumeo ana mihemko anapotazama mechi na anatamani kuvuja viti bora abaki hukohuko asije uwa njani kabisa,kipindi kilichopita walivunja viti na waliniaibisha sana sasa safari hii sintakubali kuaibishwa tena"alisema Sirro.

Akizungumzia swala la kupambana na madawa ya kulevya Sirro amesema kuwa unaposikia watanzania wamekamatwa nje ya nchi ni aibu na uharibifu mkubwa ,inaharibu sifa ya nchi yetu hivyo lazima lishughulikiwe kwa kasi kubwa.

"Vita hii ya madawa ya kulevya oparesheni yake imekuwa kubwa imegusa watu wengi ambao walidhania hawatakamatwa,wamekamatwa,mwisho wa siku tumewakamata,tunawahoji,na wakikutwa na hatia tunawapeleka mahakamani, kama aliyekamatwa hajakutwa nayo anaachiwa kwani tatizo nini jamani"alisisitiza Sirro.

Akizungumzia changamoto mbalimbali za utendaji kazi amesema kuwa ni pamoja na askari kulalamikiwa huwa linamsumbua sana kwani askari ni kioo cha jamii,uhalifu ukizidi mahali haswa ukuzingatia jeshi la polisi na wananchi wanatuamini,pamoja na taarifa za uongo ambazo hazina uhakika .

"Ninaposikia askari analalamikiwa huwa inaniumiza sana na lazima nimuite nizungumze nae na ninakuwa mkali sana katika hilo,taafifa za uongo halkadhalika tukikukamata umezusha la kuzusha huko huna uhakika kwakweli tutakushughulikia kwa mujibu wa sheria kwani umetupotezea muda kufanya uchunguzi wa jambo hilo kumbe ni uongo tu nyie ni watu wazima usiposti kitu ambacho huna uhakika nacho"alisema Sirro.

Amewataka wananchi kuacha woga pale wanapomkamata muhalifu na kumpeleka kituo cha polisi,watoe ushirikiano kwa jeshi hilo pale ambapo wanatakiwa kwenda kutoa ushahidi mahakamani,ushahidi unapokosekana mtuhumiwa huyo ataachiwa huru.

"Tatizo la watanzania wengi hawana utamaduni wa kwenda kutoa ushahidi mahakamani pale wanapohitajika,tazizo woga mwingi sana jamani Kesi ni Ushahidi na wengine wanaona wanapoteza muda,lazima atolewe ushahidi ili aweze kushtakiwa kwa mujibu wa sheria msibakie kulalamikia jeshi la polisi wamepokea rushwa".alisema

Aidha Sirro amesema kuwa hali kwa Jiji la Dar es salaam ni shwari kwa sasa ameutaja uhalifu ulioongezeka ni ubakaji na ulawiti ambapo matukio mengine kama ya poanya rod ,unyanganyi yamepungua sana,amezungumzia tukio la mauaji ya askari yaliyotokea jana ya Ofisa upelelezi wa wilaya ya Kibiti mkoa wa Pwani Peter Kubezya huko mkoa wa Pwani kibichi amesema wamejipanga kwenda kuwasaidia maana wanayo kazi kubwa ya kuhakikisha usalama wa nchi raia na mali zao ndiyo kazi ya jeshi la polisi "ukiona mwenzio amenyolewa wewe tia maji"

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : SIRRO:NINAUSONGO NA WALE WANAOFANYA FUJO ILI NIWASHUGHULIKIE KISWASWA
SIRRO:NINAUSONGO NA WALE WANAOFANYA FUJO ILI NIWASHUGHULIKIE KISWASWA
https://encrypted-tbn1.gstatic.com/images?q=tbn:ANd9GcSSc_iDk0RlDFvJRWJKzjPwpPws5M0-OkQt_86NN7TA3r5gcmZY
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/sirroninausongo-na-wale-wanaofanya-fujo.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/sirroninausongo-na-wale-wanaofanya-fujo.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy