http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

MJUE SUNGURA NA JINSI YA KUMFUGA KWA FAIDA.

Na Raymond William. Sungura!,   napolisikia jina sungura mawazo yangu yote pamoja na fikra zangu zinanipelekea kukumbuka u...










Na Raymond William.

Sungura!,  napolisikia jina sungura mawazo yangu yote pamoja na fikra zangu zinanipelekea kukumbuka ucheshi na ujanja wa mnyama huyu katika hadithi mbali mbali enzi zile nikiwa darasa la 4 katika moja ya shule za mkoa Wa Arusha. Jamanii ! nalikumbuka sanaa shahiri lile la SIZITAKI  MBICHI HIZI. Japo kuwa nakumbuka moja ya Ubeti katika shahiri lile ambalo sungura alisikika akisema.

 “SIZITAKI  MBICHI HIZI, Sungura akagumia naona nafanya kazi bila faida kujuayakamtoka machozi matunda akalilia sungura nakuambia.”  Sungura ni mnyama mwenye sifa kemkem za kuwa mjanja kuliko wanyama wote. Akuna mtoto  wa kizazi hiki ambaye apendi kufuga sungura ama ajui Hadith ya sungura na wanyama wengine.

Msomaji wangu hapa nitakwenda kukuelezea jinsi yakufuga sungura {ufugaji wa ndani} ila kuna ufugaji wanje pia lakini kwa leo tutangazia ufugaji wa ndani.  Twende sote….

Lakini Kabla hujaamua kufuga sungura hakikisha ya kwamba umejitoa na una muda wa kuwahudumia wanyama waha, ufugaji wao si rahisi kama vile ukifuga paka au mbwa, sungura wanahitaji uangalizi na hassa kwenye usafi kwa sababu ni rahisi kwao kupata maradhi yatokanayo na mazingira mabaya na machafu

Kuna aina mbili za mabanda ya kufugia kwanza ni yale ya kuwafungia ndani muda wote bila kutoka nje na ya pili ni ile ya pili ni nusu nusu yaani wanakuwa na mabanda na wanaweza kutoka nje kwenye ua maalum, katika aina zote mbili ni muhimu kuhakikisha hakuna upenyo wa kuruhusu panya kupita kwa sababu huwa wanakula watoto wa sungura.




UFUGAJI WA NDANI
1 - Usitumie banda la kioo kwa sababu halina hewa ya kutosha na ni vigumu kusafisha

2 - Sakafu ya nyavu za waya ni nzuri zaidi ila hakikisha hakuna sehemu zenye ncha kali inayoweza kuwaumiza sungura, kwani wakumia ni mpaka wapone wenyewe au umchinje kwa sababu ukitumia dawa za antibiotic sungura hana uwezo wa kuzimeng'enya na kuisha mwilini mwake, siku ukimchinja atabakia na dawa na hata ukinusa nyama yake utahisi harufu ya dawa

3 - Ukubwa wa banda usipungue mita 4 * 2 kwa kila sungura mmoja, likiwa kubwa zaidi ni vizuri

4 - Chini kuwekewe matandazio kama nyasi kavu au maranda ya mbao, lakini maranda yatokanbayo na miti yenye mafuta kama mi-pine na mikaratusi hayafai, wawekee kipande cha blanket au taulo la zamani kwa ajili ya kulalia na kujifungulia hasa kwa wazazi

5 - Ni muhimu kuwawekea sehemu ya kujificha mara wanapohisi hatari, unaweza kutumia mbao,Box gumu au plastiki



MAITAJI MUHIMU YAKUJUA KIPINDI CHA UFUGAJI.

Tumia mabakuli ya kigae, usiweke vya plastiki maana huvitafuna na kuwaathiri au jengea kwa saruji, maji yabadilishwe kila siku na vyombo visafishwe kila siku


Wapewe majani makavu kwani muhimu sana kwa ajili ya mfumo wa kumeng'enya chakula, mabaki ya mboga za jikoni baada ya kuchambuliwa, pia unaweza kuwawekea pumba au chakula cha kuku (growers mash) kwenye vyombo maalum kama chakula chenye virutubisho Kiasi cha protini wanachohitaji ni 17%

Kila siku jaribu kuondoa uchafu kama vyakula vilivyo mwagika, na kinyesi kilichoganda kwenya matandazio, fagia na kubadili matandazio angalau mara moja kwa wiki, manyoya ya sungura mzazi yasiondolewe hii huonyesha kwamba anakaribia kujifungua watoto

Wakati mwingine meno ya mbele hukua sana na kumsababishia usumbufu wakati wa kula, waone wataalam ukiona ni marefu zaidi na yanahitaji kupunguzwa, dalili kuu ni sungura kushindwa kula kwa zaidi ya masaa 12

Miguu ya sungura si kama ya wanyama wengine, nyayo zake zimefunikwa kwa manyoya, angalia ukiona yananyonyoka kuna tatizo chunguza, kucha zake zinahitaji kupunguzwa zikikua sana waone maofisa ugani wa mifugo wakusaidie kwa hili

Usimbebe kwa kutumia masiki yake huwa wanaumia sana, shika ngozi nyuma ya shingo kama paka ukitaka kumbeba na pia weka mkono mmoja kwa chini ili kusapoti uzito

Wapewe dawa ya minyoo kama piperazine kila baada ya miezi mitatu, dawa za wadudu kama akheri powdeer zinyunyuziwe kwenya mabanda yao kuzuia viroboto, usiwape dawa nyingine bila ushauri wa kitaalamu, antibiotics ndio usijaribu kabisa kama nilivyosema mwanzo

Kwa kufika hapa natumaini umepata kujua namna ya kumfuga mnyama huyu ambaye ni mjanja sana kwa tabia yake ambayo hata watoto wadogo huwapenda kwaajili ya ujanja wake tukutane tena kesho katika safu hii ya Dira kuu. KWA MAONI NA USHAURI TUPIGIE 0754954872.
                                                  www.wepesimedia.blogspot.com

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : MJUE SUNGURA NA JINSI YA KUMFUGA KWA FAIDA.
MJUE SUNGURA NA JINSI YA KUMFUGA KWA FAIDA.
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/mjue-sungura-na-jinsi-ya-kumfuga-kwa.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/02/mjue-sungura-na-jinsi-ya-kumfuga-kwa.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy