http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

MJUE MNYAMA AJULIKANEA KWA JINA LA NUNGUNUNGU

  Msomaji wa safu hii ya Dira Kuu, matumaini yangu u mzima wa afya na pole na majukumu yakulijenga taifa letu la Tanzania. Kwa mfuatiliaj...

 


Msomaji wa safu hii ya Dira Kuu, matumaini yangu u mzima wa afya na pole na majukumu yakulijenga taifa letu la Tanzania. Kwa mfuatiliaji wa makala ya dira kuu jana tulizungumzia juu ya Mnyama Aina ya Faru na tulijifunza mambo mbali mbali na siku ya leo tunaangazia juu ya mnyama Nungunungu.

Nungnungu ni wanyama wagugunaji wenye ngozi yenye miiba iliyochongoka wanayotumia kujilinda na maadui. Walienea katika ulimwengu wa sasa na ulimwengu wa zamani. Katika wanyama wagugunaji ni watatu kwa ukubwa, wakitanguliwa na capybara na buku. Nungu wana urefu kati ya sm 20 - 25. Uzito wao wakaribia kg 5.4 - 16. Wana umbo la duara, wakubwa na wataratibu kweli.
Nungunungu ni wanyama ambao huwa na rangi mbalimbali zikiwemo kijivu,nyeusi,kahawia ambayo imepauka kwa sababu ya rangi zake na kumfanya kuwa miongoni mwa vivutio vya utalii


Nungu wa dunia ya leo wanaumbo dogo (japokuwa nungunungu wa Amerika ya Kaskazini wanafikia kama sm 85 kwa maelfu na uzito wa kilogramu 18),


Ni vigumu sana kuweza kuwaona kwa vile wanaishi kwa mashaka sana,maana mara tu wanapoonekana machoni pa watu hushambuliwa na kuwaua kwa sababu mbalimbali.Wengine huwaua kwa sababu ya kuwatuhumu kuwa wanakula mazao yao mashambani.Lakini wengine huwaua kwa sababu wanadai kuwa miiba yake ni dawa.


Nungunungu hupenda kuishi na kufurahia mazingira yenye mapori na misitu ili kujihadhali na ukatilii anaotendewa.Nivigumu sana kumpata mnyama kama Nungunungu katika sehemu zenye nyasi fupi fupi huwa huishi kwe sehemu zenye nyasi ndefu kwa ajili ya usalama wao.


Nungunungu hula chakula ambacho mara nyingi hulimwa na kuandaliwa na binadamu huko mwituni,ambako ndio sehemu sahihi ya maakazi ya Nungunungu.Kutokana na kuharibiwa makazi yao Nungunungu hulazimika kula mazao yaliyolimwa kama mahindi,ndizi,mihogo,na mazao mengine yanayoliwa na binadamu hiyo upelekea kuwa na uadui mkubwa na binadamu na Nungunungu kuona kuwa mazingira alimo binadamu si maeneo sahihi kwa kuishi ns kuendeleza maisha yake yote.Kwa hiyo uhama na kwenda sehemu jingine.


Nungu hupatikana sana katika maeneo ya kawaida na tropiki ya Asia, Italia, Afrika na Amerika ya Kusini na Kaskazini. Nungu huishi kwenye misitu, jangwani sehemu zenye miamba, vilima na nyikani. Baadhi ya nungu wa Dunia Mpya huishi kwenye miti, lakini nungu wa Dunia wa Kale wanakaa ardhini. Nungu huweza kupatikana hata kwenye miamba kwenye ardhi yenye hata urefu wa mita 3700. Nungunungu ni wanyama wa usiku.


Nungunungu hawazaliani kwa wingi sana kama wanyama wengine wanaoishi mwituni hii ni kwa sababu ni wanyama ambao jamii huwatumia sana kwa ajili ya kitoweo pamoja na shughuli nyingine kama dawa ya asili.


Katika Tanzania inasemekana Nungunungu huwapatikana kwa wingi katika mapori mbalimbali likiwemo pori la Nyamunsi lililoko Wilayani Tarime Mkoa wa Mara.Baadhi ya Wenyeji wa sehemu hiyo wanaamini kuwa ngozi ya Nungunungu ni dawa ya watoto wadogo na hivyo waganga wengi huwawinda na kuwatumia kwa lengo la kutibu watu kutokana na imani tofauti katia jamii.Pia Nungunungu anahusishwa sana na uchawi kwani anaaminika kuwa ukimkuta njiani ni ishara ya kutokea kwa jambo fulani baya au zuri.


Nijukumu la sisi Watanzania kuhifadhi makazi ya wanyamapori kwa kuwa ni suala la sisi sote.Wanyamapori hawa ni urithi wetu,kila mmoja wetu atimize wajibu wake kwa nafasi yake ili kuhakikisha uwo wa rasilimali ya wanyamapori na matumizi yake vinakuwa enendelevu.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : MJUE MNYAMA AJULIKANEA KWA JINA LA NUNGUNUNGU
MJUE MNYAMA AJULIKANEA KWA JINA LA NUNGUNUNGU
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLT9LWiPctmhSORF8qRS7tFF7P7faJQErxwG4sWFRbNhdrt1WyQ96V47MnGBNk0Dmg3UUJ9iM8ECeifTxiAl8gu4MAta_YeCwdx54SXqSzH881ifpaf_9B9BOuxon66Cwxb9oWhbRtj58-/s640/photo+(2).JPG
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjLT9LWiPctmhSORF8qRS7tFF7P7faJQErxwG4sWFRbNhdrt1WyQ96V47MnGBNk0Dmg3UUJ9iM8ECeifTxiAl8gu4MAta_YeCwdx54SXqSzH881ifpaf_9B9BOuxon66Cwxb9oWhbRtj58-/s72-c/photo+(2).JPG
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2017/01/mjue-mnyama-ajulikanea-kwa-jina-la.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2017/01/mjue-mnyama-ajulikanea-kwa-jina-la.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy