http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

CHADEMA Wazua Balaa Umeya wa Kinondoni

Wakati mchakato wa uchaguzi wa meya na naibu wake ukiendelea, suala la idadi ya madiwani wa viti maalumu wa Chadema katika Manispaa ya ...




Wakati mchakato wa uchaguzi wa meya na naibu wake ukiendelea, suala la idadi ya madiwani wa viti maalumu wa Chadema katika Manispaa ya Kinondoni limeibua mvutano mpya kati ya chama hicho na ofisi ya mkurugenzi mtendaji.


Mvutano huo umejitokeza baada ya Mkurugenzi wa Kinondoni, Aron Kagurumjuli kutoa barua inayoeleza kuwa kutakuwa na madiwani viti maalumu wanawake wasiopungua theluthi moja ya madiwani wa kuchaguliwa wa Chadema.


Kwa mantiki hiyo, Chadema ambayo ina madiwani wa kuchaguliwa saba itakuwa na madiwani watatu wa viti maalumu. Kwa hiyo majina yasiyopungua matatu ndiyo yatakayowasilishwa kuunda baraza jipya la madiwani.


Hata hivyo, Katibu wa Chadema Mkoa wa Dar es Salaam, Henry Kilewo alipinga maelezo hayo ya mkurugenzi akisema: “Tayari nimeshamwandikia barua mkurugenzi kumweleza. Tungekuwa tunatoka katika uchaguzi mkuu ningekubaliana na hoja ya Kagurumjuli, lakini kwa hali ilivyo sasa siwezi kukubaliana naye kwa sababu baraza likiitishwa madiwani hawatakula kiapo kama awali.”


Kuhusu madai hayo Kagurumjuli alisema: “Nasimamia sheria, sifuati matakwa ya mtu. Nadhani wao wanapingana na sheria. Sielewi presha inatoka wapi. Wa kushinda atashinda na wa kukosa atakosa kulingana na idadi ya wajumbe wake na hakuna atakayeonewa.”


Alisisitiza kuwa kulingana na sheria hiyo na idadi ya madiwani wa kuchaguliwa wa Chadema, chama hicho hakiruhusiwi kuongeza diwani mwingine. Kagurumjuli hakuwa tayari kutaja idadi ya wajumbe watakaounda baraza la madiwani na kusema kwamba anasubiri majina ya madiwani kutoka CUF, Chadema na CCM.


Lakini Kilewo alisema msimamo wa Chadema uko palepale wa kuhakikisha madiwani wanne wanabaki Kinondoni na kwamba hakuna mwenye mamlaka ya kuengua mjumbe isipokuwa kifo na mahakama.


“Ubungo hakuna tatizo. Ingawa maelezo yanafanana ya wajumbe watatu kutakiwa kulingana na idadi ya madiwani wa kuchaguliwa. Ishu ipo Kinondoni kwa sababu madiwani wetu wa viti maalumu wengi walikubaliwa,” alisema Kilewo.


Kuhusu umeya baada ya manispaa hizo kugawanywa, Kilewo alisema jina la Mustafa Muro, Diwani wa Kinondoni, ndilo lililopendekezwa na kupelekwa kwa ajili ya kugombea umeya wa Kinondoni huku Boniface Jacob akiteuliwa kugombea Ubungo.


Wakati Kilewo akisema hayo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge alisema mchakato wa kuwapata wagombea wa nafasi ya umeya na naibu meya katika manispaa hizo ulitarajiwa kukamilika jana jioni.


“Mchakato huu ulianza muda mrefu lakini leo (jana), jioni ndiyo kilele chake. Wagombea watakaopatikana ni mahiri na CCM ipo fiti tunasubiri mechi uwanjani,” alisema Madenge.


Kwa nyakati tofauti, Manispaa za Kinondoni na Temeke zilifanya mgawanyo wa madiwani baada ya Serikali kuzigawanya na kuunda halmashauri za Ubungo na Kigamboni.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : CHADEMA Wazua Balaa Umeya wa Kinondoni
CHADEMA Wazua Balaa Umeya wa Kinondoni
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjCwnxmQR5dVzYJBRp7HHJ0guEbmBuqDM0KpxIUCSKW_Lxccy7bYG1QSHW5erc01dOL7Qy26mJauTDYBsCYg7twa8-lsW5hOPpFkwaxGHbE43oQRwG7FPOb94_-5jYgGa_FtEZMyap7xdw/s640/CHADEMA-LOGO.png
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjCwnxmQR5dVzYJBRp7HHJ0guEbmBuqDM0KpxIUCSKW_Lxccy7bYG1QSHW5erc01dOL7Qy26mJauTDYBsCYg7twa8-lsW5hOPpFkwaxGHbE43oQRwG7FPOb94_-5jYgGa_FtEZMyap7xdw/s72-c/CHADEMA-LOGO.png
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/chadema-wazua-balaa-umeya-wa-kinondoni.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/chadema-wazua-balaa-umeya-wa-kinondoni.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy