http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

BONANZA LA MWALIMU NYERERE ARUSHA LAFANA

Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akizungumza kwenye Bonanza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jiji...




Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akizungumza kwenye Bonanza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jiji Arusha,kushoto ni Afisa Michezo wa Jiji,Benson Maneno na kulia ni Katibu Tawala wa wilaya(DAS)David Mwakiposa.

Katibu Tawala wilaya ya Arusha,David Mwakiposa akizungumza kwenye Bonanza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jiji Arusha,katikati ni Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro akifatilia kwa makini na kushoto ni Afisa Michezo wa Jiji,Benson Maneno .


Katibu Tawala wilaya ya Arusha,David Mwakiposa akiangalia michoro yenye sura ya hayati Mwalimu Nyerere ilichorwa na vijana wazalendo kwenye Bonanza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jiji Arusha.

Watoto wakichuana kukimbia mbio za mita 50 kwenye Bonanza hilo.

Mkuu wa wilaya ya Arusha,Gabriel Daqarro(wa pili kushoto)akiwa na Mwenyekiti wa mchezo wa Karate mkoa wa Arusha,Richard Kitoro pamoja Sensei Dad na Sensei David wakifatilia michezo iliyokua ikiendelea.

Mmoja wa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Edmund Rice akionyesha umahiri wake kwenye mchezo wa Karate

Kikundi cha Karate kikonyesha mbinu za mchezo huo

Kikundi cha Karate kikonyesha mbinu za mchezo huo kwenye Bonanza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid jiji Arusha

Burudani nayo ilikua sehemu ya kunogesha Nyerere Day


Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Arusha kwa kushirikiana na wadau wa michezo pamoja na wananchi wa Jiji wameadhimisha siku ya Mwl. Nyerere kwa kuandaa na kushiriki kwenye Bonanza la Michezo lililopewa Jina la Bonaza la Mwalimu Nyerere lililofanyika kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid uliopo jijini hapa leo tarehe 14.10.2016.


Tamasha hili limeandaliwa maalumu kwa ajili ya kumuenzi baba wa Taifa Mwl. Julius Kambarage Nyenyere aliyefariki miaka kumi na saba iliyopita sambamba na kusherekea kilele cha Mwenge wa Uhuru ambao ulipita katika Wilaya ya Arusha mwishoni mwa mwezi wa nane na kuzindua miradi ya Afya, Maji, Elimu, Uwezeshaji wananchi, uwezeshaji makundi maalumu, Ujenzi na Usafi wa Mazingira yenye thamani ya zaidi ya TshBil 1.5.


Akiongea na wanamichezo walioshiriki katika Bonanza hilo Mkuu wa Wilaya ya Arusa Mhe. Gabriel Fabian Daqarro alisema Tamasha hili ni kwa ajili ya kumuezi Mwl. Nyenyere ambapo litasaidia vijana na wananchi kuweka miili yao safi, kujiepusha na maradhi pamoja na makundi yanayoweza kusababisha kujiingiza kwenye madawa ya kulevya, ulevi na uzururaji.


Pia tuitumie siku hii kutafakari mafundisho na maelekezo ya Mwalimu Nyerere aliyoyatoa wakati wa uhai wake, wapi Nchi imetoka, Misingi imara ya Uongozi bora na namna gani tunaweza kuenenda ili kuleta maendeleo katika Taifa letu, na vijana kama nyie ndio mnaotakiwa kuwa chachu katika kupambana na umasikini katika Nchi yetu alisema Dc Daqarro.


Naye Katibu Tawala wa Wilaya ya Arusha Bw. David Mwakiposa alielezea Tamasha hilo kuwa limeshirikisha michezo mbalimbali kama Netball, Football, Volleyball, Basketball, mchezo wa Bao, kukimbiza kuku, Baiskel, kuvuta kamba, Karate, Taekondo, Uchoraji pamoja na riadha.


Bonaza hili pia limetumika kama jukwaa la kuendelea kuelimisha na kueneza ujumbe kwa vijana kupitia kauli mbiu ya Mwenge mwaka 2016 inayosema “Vijana ni nguvu kazi ya Taifa washirikishwe na wawezeshwe”.


Nteghenjwa Hosseah
Afisa Habari, Halmashauri ya Jiji
Arusha
14.10.2016

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : BONANZA LA MWALIMU NYERERE ARUSHA LAFANA
BONANZA LA MWALIMU NYERERE ARUSHA LAFANA
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3oyBfcetuhKX361An9pZVFrUkK5QCeFzeqtlaRGjqakq-DamhV0z8C8uNmYoZeefLRm-gsqefIkoiPlhfLU3q_zJNrt_bwbTDKP-xW1SCqSP9voY4Lk0y6ggElIHpsks5m6v4rc18-beE/s640/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj3oyBfcetuhKX361An9pZVFrUkK5QCeFzeqtlaRGjqakq-DamhV0z8C8uNmYoZeefLRm-gsqefIkoiPlhfLU3q_zJNrt_bwbTDKP-xW1SCqSP9voY4Lk0y6ggElIHpsks5m6v4rc18-beE/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/bonanza-la-mwalimu-nyerere-arusha-lafana.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/10/bonanza-la-mwalimu-nyerere-arusha-lafana.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy