http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

post-feature-image

NSSF Yaburuzwa Mahakamani


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limeburuzwa mahakamani na wakazi 87 waliokopeshwa nyumba za mradi wa shirika zilizoko Kijich...

Polisi wazuia ghafla mkutano wa CHADEMA Chalinze........Mbowe Asema Wapo Tayari Kufa Kwa Kupigania Demokrasia
Mama Mwenye VVU Pamoja na mtoto wake wakutwa wamekufa mlimani
Tundu Lissu Akamatwa na Jeshi la Polisi Akiwa Singida.....Msigwa Ahutubia Iringa, Adai Serikali Imekurupuka Kuhamia Dodoma


SHIRIKA la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), limeburuzwa mahakamani na wakazi 87 waliokopeshwa nyumba za mradi wa shirika zilizoko Kijichi jijini Dar es Salaam, wakiiomba lisiwabugudhi hadi kesi ya msingi itakaposikilizwa. 

 Kesi hiyo imefunguliwa na wakazi hao katika Mahakama Kuu Divisheni ya Ardhi, wakilalamikia Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF na Kampuni ya Majembe Auction Mart. Kesi hiyo ilipangwa kutajwa jana mbele ya Jaji Penterine Kente. 

 Wakili wa walalamikaji hao, Benito Mandele, amewasilisha maombi mahakamani hapo kutaka itoa amri ya kutokubugudhiwa na mazingira ya makazi hayo yabaki kama yalivyo hadi kesi yao ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi. 

Katika kesi ya msingi, mbali na NSSF, mlalamikiwa wa pili ni Majembe ambaye hakufika mahakamani. Wakili Mandele alidai kuwa alipeleka wito wa mahakama katika ofisi yake iliyoko Mwenge, lakini hakufanikiwa kumpata kwa kuwa amehamisha ofisi eneo hilo. 

Jaji Kente alisema mahakama inatoa hati nyingine kwa ajili ya mlalamikiwa wa pili ili afike mahakamani kusikiliza kesi dhidi yake. Kesi ya msingi itasikilizwa Oktoba 17, mwaka huu, na maombi ya kutokubughudhiwa yatasikilizwa Agosti 24, mwaka huu.

Wakazi hao kupitia kwa wakili wao, waliamua kukimbilia mahakamani kufungua shauri hilo, baada ya kushindwa kupata ufumbuzi wa madai yao katika Taasisi ya Usuluhishi kutokana na walalamikiwa kutofika. 

Ilidaiwa kuwa wakazi hao waliamua kwenda katika taasisi ya usuluhishi kutokana na mkataba wao kuwataka kufanya hivyo kabla ya kuamua kwenda mahakamani. 

Kwa mujibu wa hati ya madai, wakazi hao wanadai kwamba mlalamikiwa wa kwanza (Bodi ya Wakurugenzi ya NSSF), ameshindwa kutekeleza makubaliano kwa mradi huo kukosa huduma za kijamii. 

Aidha, wanadai nyumba hizo hazina ubora hali iliyowalazimu wengi wao kutumia fedha zao kufanya ukarabati. 

Wanadai kuwa kutokana na hali hiyo, baadhi ya wakazi wameshindwa kulipa fedha ambazo wanatakiwa kulipa kila mwezi, hivyo Majembe walifika na kuwapatia notisi na kuwatangazia kuwaondoa. 

Wakazi hao wanaiomba mahakama hiyo, kuiamuru bodi hiyo kurejea mikataba, kutambua majukumu ya msingi ya kila upande na nyumba ziwe za kuwawezesha kuishi na kuwe na huduma za kijamii. 

Katika maombi, wakazi hao wanaiomba mahakama hiyo kutoa amri ya hali ilivyo kwa wakazi hao katika makazi hayo ibaki kama ilivyo mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa na kutolewa uamuzi.

Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : NSSF Yaburuzwa Mahakamani
NSSF Yaburuzwa Mahakamani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjtzc0SEX7jHzWjxLrHLH_weWDT7yK9majN1X40RIwnb8EIkXSS8-l8ZSHV5522AMFnA9HXNg18ESjG5iBJlgFLz9-OTia_5fWjrQybyORMmBev7LcHbke_kLNiYxfBakiuXNX51tfEilk/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjtzc0SEX7jHzWjxLrHLH_weWDT7yK9majN1X40RIwnb8EIkXSS8-l8ZSHV5522AMFnA9HXNg18ESjG5iBJlgFLz9-OTia_5fWjrQybyORMmBev7LcHbke_kLNiYxfBakiuXNX51tfEilk/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/nssf-yaburuzwa-mahakamani.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/nssf-yaburuzwa-mahakamani.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy