http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mtuhumiwa Auawa Ndani ya Kituo cha Polisi

MKAZI wa Kwere wilayani Babati Mkoa wa Manyara, Mohamedy Pagweje (29), amepigwa na kufa na mtu anayedaiwa kuwa hana akili timamu aliye...


MKAZI wa Kwere wilayani Babati Mkoa wa Manyara, Mohamedy Pagweje (29), amepigwa na kufa na mtu anayedaiwa kuwa hana akili timamu aliyewekwa naye katika chumba cha mahabusu katika Kituo cha Polisi cha Mkoa wa Manyara, kilichopo wilayani Babati.

Hata hivyo, ndugu wa Pagweje ambaye ni fundi ujenzi wa eneo hilo, wamekataa kuuchukua mwili kwa maziko wakitaka kujua ukweli wa kifo chake baada ya kupigwa akiwa mahabusu katika Kituo cha Polisi cha Babati.

Mama mzazi wa kijana huyo Hadija Pagweje, akizungumza na waandishi wa habari jana nje ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya hiyo, Raymond Mushi, alisema alimkabidhi mtoto wake kituoni hapo saa 8:00 mchana juzi akiwa salama.

Alisema alimfikisha mwanawe kituoni hapo baada ya kijana huyo kulewa pombe na kutishia kujiua kutokana na kutolipwa fedha za ujenzi kutoka kwa askari aliyemjengea nyumba. Askari huyo ametajwa kwa jina moja la Justine.

“Nilimwacha hapa kituoni mahali pa usalama na kuwaomba askari wa zamu wanisaidie maana kijana wangu amekunywa pombe nyingi, anatishia kujiua kwa madai kuwa amekosa haki yake. Nilifanya hivyo nikijua kituo cha polisi kina usalama ili angalau pombe ziishe, jioni nimchukue,” alisema.

Alipokwenda kupeleka chakula polisi walimtaka arudi tena saa 12:00 jioni, aliporudi kituoni hapo alishangaa kuona baadhi ya watu wakimshangaa na kumjulisha kuwa kijana wake amepigana na mahabusu mwenzie na kuwa amepelekwa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Babati ya Mrara kwa matibabu.

Alisema alipokwenda katika hospitali hiyo alikutana na askari ambaye alimfahamisha kuwa mtoto wake alikuwa amefariki dunia. Baba wa marehemu Amiri Shabani alisema alipata taarifa ya kifo cha kijana wake saa 1:00 usiku juzi baada ya kuelezwa kuwa mtoto wake alikufa akiwa anadai Sh 200,000 kutoka kwa askari huyo.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Francis Massawe alikiri kutokea kwa tukio hilo, saa 8:00 mchana Agosti 8, mwaka huu ambapo alisema mama wa marehemu alimpeleka kituoni hapo kijana wake Pagweje, fundi ujenzi akidai kuwa alikuwa akimletea fujo na alifunguliwa mashtaka ya kutishia kuua.

Alipoingizwa mahabusu alipigana na mahabusu mwenzake Bura Malireh (19) mkulima na mkazi wa Gijedaboung Kata ya Mamire wilayani humo, ambaye ilidaiwa alikuwa mgonjwa wa akili.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mtuhumiwa Auawa Ndani ya Kituo cha Polisi
Mtuhumiwa Auawa Ndani ya Kituo cha Polisi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcyBVHfcodvXuN_k_xQjhPeKqw_K1Uw-9B_EcmSqSNzIprCEuXhpUsxO4abICDzc57daI5Hp9uF0bRSSn2UDexo5NQB6Gt7xxlvL9a2jNp5StgYrCQEU9d6aocA5vKQ162oYjSwN2NWXU/s1600/polis.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhcyBVHfcodvXuN_k_xQjhPeKqw_K1Uw-9B_EcmSqSNzIprCEuXhpUsxO4abICDzc57daI5Hp9uF0bRSSn2UDexo5NQB6Gt7xxlvL9a2jNp5StgYrCQEU9d6aocA5vKQ162oYjSwN2NWXU/s72-c/polis.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/mtuhumiwa-auawa-ndani-ya-kituo-cha.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/08/mtuhumiwa-auawa-ndani-ya-kituo-cha.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy