http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Samsung yafeli mtihani wa kuwa ndani ya maji

Simu ya kisasa ya Samsung Galaxy S7 inayopigiwa upatu kuwa na uwezo wa kustahimili kuwa chini ya maji imefeli majaribio ya shirika la mo...

Simu ya kisasa ya Samsung Galaxy S7 inayopigiwa upatu kuwa na uwezo wa kustahimili kuwa chini ya maji imefeli majaribio ya shirika la moja la kutathmini ubora wa bidhaa za kielektroniki.
Programu ya simu hiyo ya Samsung Active ilizima punde baada ya kutumbukizwa ndani ya pipa la maji.
Kampuni hiyo ya kutathmini ubora wa bidhaa, Consumer Reports ilirejelea jaribio hilo kwa mara ya pili wakitumia simu tofauti na kama ile ya kwanza ikafeli.
Kampuni ya kutengeza simu hiyo ya Samsung ikijitetea imesema huenda simu hizo zilikuwa ni mbovu na hivyo kuruhusu maji kuingia ndani.

Simu hizo zilitumbukizwa ndani ya mapipa ya maji na kutolewa baada ya dakika.
Simu hizo za Samsung zilizima.
Kulikuwa hata na maji katika eneo la kamera za simu hizo mbali na viputo.

Kampuni inayotengeza simu hizo kutoka Korea Kusini Samsung imejitetea vikali ikisema kuwa Galaxy S7 Active, inayouzwa Marekani imefanyiwa majaribio kabambe na hata kupewa cheti maalum cha IP68.
Hati hiyo maalum inathibitisha kuwa simu hizo zinauwezo wa kustahimili kutumbukizwa ndani ya maji.
Consumer Reports iligonga vichwa vya habari kote duniani ilipotambua kuwa simu aina ya Iphone 4 ilikuwa na matatizo ya ya kifaa cha kuungia mbali.
''kwa kawaida tumekuwa tukiamini pale mtengezaji wa bidhaa akituambia kuwa bidhaa yake inaweza kustahimili hata kutumbukizwa ndani ya maji, lakini leo tulipojaribu kuhakiki madai ya Samsung tuligundua kuwa simu hizo zinazima baada ya kutumbukizwa ndani ya pipa la maji ''
''Bila shaka wale walionunua simu hizo kwa imani kuwa haitoharibika hata baada ya kutumbukizwa ndani ya maji, watalazimika kutafuta ridhaa kutoka kwa watengenezaji,,,''

Simu hiyo ilianza kuuzwa mwezi juni mwaka huu.
Mwaka uliopita Sony, iliwaonya watumiaji wa bidhaa zake kuwa kulikuwa na uwezekano kuwa simu zake zitaharibika zikitumika ndani ya maji.
Samsung inatarajiwa kutangaza faida kubwa zaidi baada ya mauzo yaliyozidi matarajio ya simu hiyo aina ya Galaxy S7.

TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Samsung yafeli mtihani wa kuwa ndani ya maji
Samsung yafeli mtihani wa kuwa ndani ya maji
http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2016/03/15/160315132936_samsung_galaxy_s7_edge_624x351_getty_nocredit.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/samsung-yafeli-mtihani-wa-kuwa-ndani-ya.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/samsung-yafeli-mtihani-wa-kuwa-ndani-ya.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy