http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mabaki ya Wafilisti yapatikana Israel

Watafiti wanasema hilo ni kaburi la kwanza kabisa la Wafilisti kupatikana   W...

Wafilisti
Watafiti wanasema hilo ni kaburi la kwanza kabisa la Wafilisti kupatikana
 
Watafiti wa mambo ya kale nchini Israel wamegundua makaburi ya kwanza ya Wafilisti.Makaburi hayo, yaliyopatikana eneo la Ashkelon, yaligunduliwa mwaka 2013, lakini habari hizo zilifichuliwa Jumapili.
Habari hizi ziliwekwa siri muda huo wote kuzuia kushambuliwa na waandamanaji wa makundi ya Wayahudi wahafidhina ambao hawakutaka makaburi hayo yafukuliwe.
  Mradi
                          Mradi wa Leon Levy ulianzishwa miaka 30 iliyopita
Taarifa zinasema ugunduzi huo huenda ukafichua mengi kuhusu asili ya Wafilisti ambao wamezungumziwa sana katika vitabu vya kidini.
Mafanikio hayo yalitokea mwisho wa mwaka wa 30 wa uchimbaji ulioongozwa na kundi la Leon Levy Expedition.
Viongozi wa uchimbaji huo wanasema walipata makaburi yaliyozingirwa na manukato, vyakula, mapambo, vito na silaha.
Yanadaiwa kujengwa na kutumiwa kati ya karne ya 11 na karne ya 8 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.

"Baada ya kutafiti kuhusu Wafilisti kwa miongo mingi, hatimaye tunaweza kuwatazama,” anasema mmoja wa wanaakioloiia hao Daniel M Master.
“Kwa ugunduzi huu, tunakaribia kubaini siri za asili yao.”
Wanaakiolojia hao sasa wanafanya uchunguzi wa DNA pamoja na uchunguzi wa miale ya ukaa kubaini watu hao waliishi wakati gani.
Lawrence E. Stager
Profesa Lawrence E. Stager ni mmoja wa wanaoongoza utafiti huo

Watafiti hutofautiana kuhusu asili ya Wafilisti, baadhi wakiamini walitoka Ugiriki, wengine visiwa vya Crete au Cyprus na wengine eneo la Anatolia nchini Uturuki.
Wafilisti huoneshwa katika Biblia kama maadui wakuu wa Waisraeli, na inadhaniwa walihamia Israel kutoka maeneo ya Magharibi karne ya 12 kabla ya kuzaliwa kwa Yesu.

Anayefahamika zaidi ni Goliath, mpiganaji ‘jitu’ ambaye kwa mujibu wa Biblia, aliuawa na Daudi kabla yake kuwa Mfalme wa Waisraeli.
Katika Biblia, wanaoneshwa kama watu wakatili lakini mabaki yaliyopatikana yanaonekana kuashiria kwamba walikuwa na ustaarabu fulani.

TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mabaki ya Wafilisti yapatikana Israel
Mabaki ya Wafilisti yapatikana Israel
http://ichef-1.bbci.co.uk/news/ws/624/amz/worldservice/live/assets/images/2016/07/11/160711063855__philistine_640x360_afp_nocredit.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/mabaki-ya-wafilisti-yapatikana-israel.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/07/mabaki-ya-wafilisti-yapatikana-israel.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy