Gari lililokuwa limetegwa vilipuzi lililipuka karibu na lango la kiwanda cha gesi. Kumetokea shambulizi la kujitolea...
| Gari lililokuwa limetegwa vilipuzi lililipuka karibu na lango la kiwanda cha gesi. |
Kumetokea shambulizi la kujitolea Mhanga katika kiwanda cha gesi kaskazini mwa mji mkuu wa Iraq, Baghdad.
Msemaji wa jeshi la Iraq anasema gari lililokuwa limetegwa vilipuzi lililipuka karibu na lango la kiwanda hicho.
Baadaye washambuliaji sita wa kujitolea kufa wakaingia ndani ya kiwanda hicho ambapo walikabiliana na maafisa wa uslama.
Matenki ya gesi pia yamewashwa moto.



