http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Rais ashtukiza uwanja wa ndege Dar

RAIS John Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja dhidi ya dosari za u...


RAIS John Magufuli ameiagiza Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi na vyombo vya dola kuchukua hatua mara moja dhidi ya dosari za ukaguzi zilizopo katika kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere (Terminal One) jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, Ikulu, Gerson Msigwa ilisema Rais Magufuli alitoa agizo hilo jana, alipofanya ziara ya kushtukiza katika uwanja huo na kubaini kuwa mashine za ukaguzi za sehemu ya kuwasili abiria na mizigo, hazifanyi kazi kwa muda mrefu.

Maofisa wa uwanja huo waliokuwa wakitoa maelezo juu ya hali ya kitengo cha ukaguzi wa mizigo na abiria katika uwanja huo, walikuwa wakitoa taarifa zinazotofautiana kuhusu utendaji kazi wa mashine za ukaguzi, hali iliyosababisha Rais Magufuli aamue kuiagiza wizara husika kwa kushirikiana na vyombo vya dola, kuchukua hatua mara moja.

“Unajua mimi sipendi kudanganywa, ni vizuri uzungumze ukweli tu, kwa nini nimeanzia hapa huwezi ukajiuliza? Eeeh sasa sipendi kudanganywa, ukinidanganya nitachukia sasa hivi, wewe umenidanganya kwamba hiyo ndio mbovu na hii ndio nzima, nikawaambia muiwashe hiyo nzima, akaja huyu mwenzako amezungumza ukweli kabisa, akasema hii ni mbovu kwa miezi miwili.

“Kwa hiyo mizigo inayoingia humu huwa hamuikagui kwa namna yoyote ile, kwa hiyo mtu nikiamua kuja na madawa yangu ya kulevya, nikaja na dhahabu zangu, na almasi zangu na meno ya tembo kwa kutumia hizi ndege ndogondogo napita tu,” alisema Rais Magufuli kwa maofisa hao wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere.

Rais Magufuli alifanya ziara hiyo ya kushtukiza baada ya kuwasili katika uwanja huo akitokea jijini Kampala nchini Uganda, ambako juzi alihudhuria sherehe ya kuapishwa kwa Rais wa Uganda, Yoweri Museveni.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Rais ashtukiza uwanja wa ndege Dar
Rais ashtukiza uwanja wa ndege Dar
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh58-vrtsHpyE4l7AbGSxb1IALoj_h_9v9yzohOz5kem_EWCgPbnVc_LXIkYTUhNPROBCLtxeYEZCI1RmqwgT_3YPT7bzf65QbxkM7KMUzFDVPum7Ft8mwrbGmq5b0dN6xHlahEds3eLLH2/s400/rais-magufuli1_210_120.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEh58-vrtsHpyE4l7AbGSxb1IALoj_h_9v9yzohOz5kem_EWCgPbnVc_LXIkYTUhNPROBCLtxeYEZCI1RmqwgT_3YPT7bzf65QbxkM7KMUzFDVPum7Ft8mwrbGmq5b0dN6xHlahEds3eLLH2/s72-c/rais-magufuli1_210_120.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/rais-ashtukiza-uwanja-wa-ndege-dar.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/05/rais-ashtukiza-uwanja-wa-ndege-dar.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy