http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Serikali mpya ya umoja yaundwa Sudan Kusini

Makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amelivunja bunge lake na kuunda serikali ya umoja, katika har...

Makubaliano ya amani nchini Sudan Kusini
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amelivunja bunge lake na kuunda serikali ya umoja, katika harakati za kupiga jeki makubaliano ya amani yanayolenga kumaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vya takriban miaka miwili.

Mpango huo unaowashirikisha waliokuwa waasi katika serikali ulitangazwa Alhamisi katika runinga ya taifa.

Thuluthi moja ya mawaziri wa bunge hilo jipya ni wanachama wa chama cha SPLM-IO kilichobuniwa na aliyekuwa kiongozi wa waasi Riek Machar,ambaye alirudi mjini Juba mapema wiki hii ili kuapishwa kuwa makamu wa kwanza wa rais.





Makumi ya maelfu wameuawa na watu milioni 2 wakiwachwa bila makao katika mgogoro huo wa Sudan Kusini ambayo ilipata uhuru wake mwaka 2011.


Mwandani wa rais Salva Kiir Kuol Manyang atasalia kuwa waziri wa Ulinzi na David Deng Athorbei akiwa waziri wa fedha ambao watajaribu kuimarisha uchumi ulioathiriwa na vita vya zaidi ya miaka miwili.
Wizara muhimu ya mafuta ilipewa Dak Duop Bichok.
Riek Machar na Salva Kiir
Wizara ya kigeni imechukuliwa na Deng Alor wadhfa alioshikilia chini ya serikali moja ya Sudan kabla ya Sudan Kusini kupata uhuru wake mwaka 2011.

Alor alikuwa mwanachama wa kundi linalojiita ''wafungwa wa zamani'',viongozi wenye ushawishi waliokamatwa wakati vita vilipoanza,lakini baadaye wakaachiliwa baada ya shinikizo kali.

Kiongozi wa upinzani na mkosoaji mkubwa Lam Akol atakuwa waziri wa kilimo na usalama wa chakula,ikiwa ni wizara muhimu ambapo watu milioni tano wanahitaji msaada,huku maeneo mengine yakikabiliwa na ukame.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Serikali mpya ya umoja yaundwa Sudan Kusini
Serikali mpya ya umoja yaundwa Sudan Kusini
http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2016/04/29/160429092915_south_sudan_peace_512x288_bbc_nocredit.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/serikali-mpya-ya-umoja-yaundwa-sudan.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/serikali-mpya-ya-umoja-yaundwa-sudan.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy