http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Mwenyekiti CCM Arusha alalamikia hujuma

mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Michael Lekuler MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Arusha, Michael Lekule Laizer amemuony...

mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Michael Lekuler
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Arusha, Michael Lekule Laizer amemuonya Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Mosses Mabula kushiriki vitendo vya hujuma katika halmashauri hiyo.

Baadhi ya hujuma hizo zinazodaiwa kufanywa na halmashauri hiyo inayoongozwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) ni pamoja na kuzinyima miradi kata zinazoongozwa na madiwani wa CCM.

Laizer ametoa tahadhari hiyo mjini hapa jana katika kata ya Mangola Barazani alipokuwa akizungumza katika mkutano wa ndani na viongozi wa chama wa ngazi za matawi na kata kuhusu kero mbalimbali za wananchi wa kata hiyo.

Mwenyekiti huyo alifikia hatua hiyo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa diwani wa kata hiyo kupitia CCM, Lazaro Emanuel.

Emanuel alisema kwa kipindi kirefu tangu ameingia madarakani amekuwa akikosa ushirikiano kutoka kwa uongozi wa halmashauri hiyo akiwepo pia mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Mabula na hadi sasa hajakubaliwa ombi la mradi hata mmoja.

Alisema hali hiyo haijaishia kwake tu bali kwa madiwani wengine wa CCM kutoka kata zingine ambapo pia wamekuwa wakitengwa katika baadhi ya vikao hususan vya kuandaa bajeti ya halmashauri hiyo na madiwani wa Chadema wamekuwa wakiitana katika vikao vichochoroni na kuandaa bajeti kisha wao hutaarifiwa ikiwa imeshafikishwa hazina.

Alisema hata bajeti iliyopelekwa hivi karibuni hazina wao kama madiwani wa CCM hawakuifahamu wala kushirikishwa mapema bali wamekuja kuambiwa waijadili wiki tatu tangu kufikishwa hazina ilipoandaliwa na madiwani wa Chadema pekee na mkurugenzi huyo, jambo lililowasababisha madiwani hao kususia baraza hilo na kutoka nje ya kikao.

Akijibu hayo, Laizer alimtaka diwani huyo kuitisha mikutano ya wananchi wake na kuwaeleza juu ya hujuma hizo ili wazitambue.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Mwenyekiti CCM Arusha alalamikia hujuma
Mwenyekiti CCM Arusha alalamikia hujuma
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjelISrNwIcLDu0DBOpf2CMS1k1vNr5KwtX8JYk5YEpIDhbqTRSCP70AIN4mDfeepWLTE_3mGLgf97WOV9D8i5CBz39QjITz7E4xgsMb52LGZVQUWoDUv43ZNyx8BvzOZ0eMbwtszy6JzZC/s320/lekule-laizer_210_120.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjelISrNwIcLDu0DBOpf2CMS1k1vNr5KwtX8JYk5YEpIDhbqTRSCP70AIN4mDfeepWLTE_3mGLgf97WOV9D8i5CBz39QjITz7E4xgsMb52LGZVQUWoDUv43ZNyx8BvzOZ0eMbwtszy6JzZC/s72-c/lekule-laizer_210_120.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/mwenyekiti-ccm-arusha-alalamikia-hujuma.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/mwenyekiti-ccm-arusha-alalamikia-hujuma.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy