http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

CUF kudai haki kwa amani

KATIBU MKUU WA CUF MSALIM SEIF SHARIFF HAMAD CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesisitiza kuwa kitaendelea na juhudi za kutafuta haki yake kwa...

KATIBU MKUU WA CUF MSALIM SEIF SHARIFF HAMAD
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimesisitiza kuwa kitaendelea na juhudi za kutafuta haki yake kwa njia yoyote, lakini ya amani ambayo itaungwa mkono na wananchi wa Zanzibar na kwa kuanzia wametangaza kutoitambua Serikali itakayoundwa na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.

Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad aliwataka wananchi na wafuasi wa chama hicho kuwa watulivu katika kipindi hiki ambacho alisema CUF ipo katika juhudi za kutafuta haki wanayodai ilitokana na kushinda katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka jana ambao ulifutwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC).

Maalim Seif alisema hayupo tayari kukaa meza moja na Dk Shein kwa ajili ya kutafuta suluhu ya Zanzibar.
“Sipo tayari kukutana na Shein Ikulu kwa ajili ya mazungumzo ya kuleta amani na utulivu Zanzibar...... nitakutana na yeye kama nani kwa sababu sisi CUF hatutambui ushindi wa Shein katika uchaguzi wa marudio pamoja na serikali yake,” alisema Maalim Seif aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais katika Serikali ya Umoja wa Kitaifa.

Aidha, Baraza Kuu la CUF limepitisha maazimio ya kuunga mkono uamuzi wa Marekani kuinyima Tanzania msaada kupitia Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) hivi karibuni.

Kwa upande wake, Chama Cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar kimeipongeza Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China kwa juhudi zake ikiwemo kuiunga mkono Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika juhudi zake za kuleta maendeleo kwa wananchi wake na miradi ya maendeleo.

Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Vuai Ali Vuai aliwaambia waandishi wa habari jana kuwa Serikali ya Watu wa China ni miongoni mwa nchi marafiki makubwa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mara baada ya nchi mbili kuwa Jamhuri viongozi wake walikuwa marafiki wakubwa wakitembeleana na kubadilisha wataalamu.

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : CUF kudai haki kwa amani
CUF kudai haki kwa amani
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhEPpeFODWjf6oYRj_3LvPo5KaIQu_Z1dNUFwN31T3YLhwB6ccTiQFU9ringwyXmcLedCBgq7wgSquNIB9s9velzo5k_-Nfq-LNQrvAfla8SKHumxoxmYixsIG3fVy1UMrjSWlNFzOSTG-8/s1600/seif-sharif-hamad_210_120.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhEPpeFODWjf6oYRj_3LvPo5KaIQu_Z1dNUFwN31T3YLhwB6ccTiQFU9ringwyXmcLedCBgq7wgSquNIB9s9velzo5k_-Nfq-LNQrvAfla8SKHumxoxmYixsIG3fVy1UMrjSWlNFzOSTG-8/s72-c/seif-sharif-hamad_210_120.jpg
WEPESI MEDIA
https://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/cuf-kudai-haki-kwa-amani.html
https://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2016/04/cuf-kudai-haki-kwa-amani.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy