http://wepesimedia.blogspot.com/p/blog-page.html

Alieua mateka afa akiwatoroka polisi

Jeshi  la Polisi Mkoa wa Geita, limemuua kwa kumpiga risasi mtu anayedhaniwa kuwa kiongozi wa kundi la watekaji na wauaji wa watu wanao...

Jeshi  la Polisi Mkoa wa Geita, limemuua kwa kumpiga risasi mtu anayedhaniwa kuwa kiongozi wa kundi la watekaji na wauaji wa watu wanaotekwa kwa lengo la kujipatia fedha.

Polisi ilisema jana kuwa mtu huyo aliuawa wakati alipojaribu kuwatoroka punde baada ya kuonyesha mashimo mawili yaliyokuwa na miili ya watu aliowaua baada ya kuwateka.

Akizungumza na waandishi wa habari jana ofisini kwake mjini Geita, Kamanda wa Polisi Mkoa, Mponjoli Lotson alimtaja marehemu huyo kuwa Panda Kinasa.

Alisema aliuawa juzi wilayani Bukombe mkoani Geita kwa kupigwa risasi baada ya kupewa onyo na kukaidi kusimama.

Kamanda Mpojoli alisema Kinasa alipigwa risasi kwenye tako na alifaraiki dunia wakati akikimbizwa kwenda Hospitali ya Bukombe, kutokana na kupoteza damu nyingi.

Mwezi uliopita katika nyakati tofauti, alisema kamanda huyo, mtuhumiwa alivamia nyumba ya mfugaji Mbuga Siga katika kijiji cha Ikuzi Lunzewe wilayani Mbogwe usiku wa saa tatu na kumteka mchunga ng'ombe wake Renard Samwel mwenye umri wa miaka 18.

Akisimulia zaidi, Kamanda Mponjoli alisema baada ya kutekeleza utekaji huo, mtuhumiwa aliacha karatasi yenye ujumbe na namba ya simu 0752 901908 akielekeza kutumiwa Sh. milioni 2 kwenye namba hiyo ili aweze kumuachia huru mateka.

"Familia ilitoa taarifa polisi na kufunguliwa jalada ambapo upelelezi ulianza kwa kufuatilia namba hiyo kupitia kitengo maalum cha Jeshi la Polisi kinachohusiana na makosa ya uhalifu wa mitandao ili kubaini alipo mtuhumiwa," alisema.

Wakati polisi ikiendelea na upelelezi wa tukio hilo, Mei 7 saa saba za usiku mtuhumiwa alivamia tena katika kitongoji cha Bwendaseko, Kijiji cha Buganzu wilayani Bukombe na kumteka Nkwambi Mwandu (25), alisema kamanda huyo.

Baada ya utekaji huo pia aliacha ujumbe na namba ile ile 0752 901908 ukielekeza atumiwe Sh. milioni 7 ili aweze kumuachia Nkwambi, alisema.

Kamanda Mponjoli alisema familia ya Nkwambi ilimudu kutuma Sh. 500,000 kwa mpesa na kisha kuripoti Polisi.

Kutokana na ripoti ya pili hiyo iliilazimu kuendeshwa operesheni maalum ambapo Mei 31 polisi walifanikiwa kumnasa mtuhumiwa kupitia mtandao na baada ya kuhojiwa alikiri kuhusika na matukio yote mawili, alisema.

"Baada ya kumkamata mtuhumiwa alikiri na kuwapeleka makachero wa polisi katika msitu uliopo Kijiji cha Msasa na kisha kuwaonyesha shimo lenye urefu wa zaidi ya futi 20 ambamo mwili wa Renard Samwel ulikuwa umetupwa na kutelekezwa," alisema Kamanda Mponjoli. Mwili huo umetambuliwa na ndugu zake.

Mtuhumiwa Kinasa anayedaiwa na polisi kuwa na ujuzi na ubobezi katika matumizi na kucheza na mtandao wa simu, alidai alimuua Samwel baada ndugu zake kushindwa kumtumia fedha aliyokuwa ameomba ili aweze kumuachia.

"Baada ya kuonyesha mwili huo mtuhumiwa aliwapeleka tena (polisi) katika shimo jingine katika msitu uliopo katika kitongoji cha Ibogolre wilayani Mbogwe na kuwaonyesha mwili wa marehemu Nkwabi Mwandu uliokuwa umetupwa na kutelekezwa kwenye shimo lenye urefu wa zaidi ya futi 30," alisema kamanda huyo na kwamba "nao umetambuliwa na ndugu zake."

Baada ya kuonyesha miili yote miwili, mtuhumiwa Kinasa alimpinga kikumbo mmoja wa askari aliokuwa nao na kuanza kukimbia kwa lengo la kutoroka, alisema zaidi Kamanda Mponjoli na kwamba hata baada ya kupewa onyo la kusimama, alikaidi na ndipo polisi walipomfyatulia risasi na kumpiga takoni.

Mwili wake umehifadhiwa katika Hosptali ya Wilaya ya Bukombe na polisi inaendelea na upelelezi ili kuwatambua washirika wa mtuhumiwa, alisema.
Credit: Nipashe

COMMENTS


TANGAZA NASISI KWA BEI NAFUU NA UPATE MATOKEO MAZURI KATIKA BIASHARA YAKO.

MAGAZETI$type=sticky$count=4


Name

BIASHARA NA UCHUMI BREAKING NEWS BURUDANI ENGLISH NEWS GOSIIP GOSPEL HABARI HABARI PICHA MAGAZETI MAKALA MATUKIO MICHEZO MUSIC VIDEO WAZO LANGU
false
ltr
item
WEPESI MEDIA : Alieua mateka afa akiwatoroka polisi
Alieua mateka afa akiwatoroka polisi
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgr2YzdxdfWIiJALSURea5nHFlUK2VGWYsS2Rbq-1vuccu2fx22jy_CCpVRB08uTCn8lCrRGfdwejEKKyjpO7W-dbaEmtJtMCjntvE2DeyJOyhbL24uOWhDMMKIOGt_Q-QeeJpWuznVqqqJ/s1600/1.jpg
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgr2YzdxdfWIiJALSURea5nHFlUK2VGWYsS2Rbq-1vuccu2fx22jy_CCpVRB08uTCn8lCrRGfdwejEKKyjpO7W-dbaEmtJtMCjntvE2DeyJOyhbL24uOWhDMMKIOGt_Q-QeeJpWuznVqqqJ/s72-c/1.jpg
WEPESI MEDIA
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/alieua-mateka-afa-akiwatoroka-polisi.html
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/
http://wepesimedia.blogspot.com/2018/06/alieua-mateka-afa-akiwatoroka-polisi.html
true
925270315725722404
UTF-8
Not found any posts VIEW ALL Readmore Reply Cancel reply Delete By Home PAGES POSTS View All

USIPITWE NA HIZI HAPA CHINI LABEL ARCHIVE SEARCH ALL POSTS Not found any post match with your request Back Home Sunday Monday Tuesday Wednesday Thursday Friday Saturday Sun Mon Tue Wed Thu Fri Sat January February March April May June July August September October November December Jan Feb Mar Apr May Jun Jul Aug Sep Oct Nov Dec just now 1 minute ago $$1$$ minutes ago 1 hour ago $$1$$ hours ago Yesterday $$1$$ days ago $$1$$ weeks ago more than 5 weeks ago Followers Follow THIS CONTENT IS PREMIUM Please share to unlock Copy All Code Select All Code All codes were copied to your clipboard Can not copy the codes / texts, please press [CTRL]+[C] (or CMD+C with Mac) to copy